Home » » WALIMU WA SEKONDARI TANDAHIMBA WAPEWA MOTISHA UFAULU MZURI WA WANAFUNZI KIDATO CHA PILI NA KIDATO CHA NNE.

WALIMU WA SEKONDARI TANDAHIMBA WAPEWA MOTISHA UFAULU MZURI WA WANAFUNZI KIDATO CHA PILI NA KIDATO CHA NNE.


Julai 24,2024

Walimu wa Shule za Sekondari Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba waliofanya vizuri katika matokeo ya Mitihani ya upimaji ya Kitaifa kidato Cha Pili na  Kidato Cha Nne  wamepongezwa na kupewa zawadi na vyeti ikiwa ni sehemu ya motisha kuendelea kufanya Vizuri.

Akimkabidhi zawadi hizo Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Francis Mkuti amewapongeza walimu hao na Shule zilizofanya vizuri akisisitiza ari na Kasi ya kuongeza ufaulu .

Aidha, Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Tandahimba Sosthenes Luhende amesema zawadi hizo zimetolewa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji na kugawiwa katika makundi ya Shule zilizofanya vizuri, Walimu waliofaulisha Wanafunzi kwa ufaulu wa juu pamoja na Utunzaji Bora wa Mazingira ya Shule .
#kaziiendeleešŸ”„šŸ”„

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa