Home » » KAMATI YA FEDHA TANDAHIMBA YARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

KAMATI YA FEDHA TANDAHIMBA YARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

Agosti 5, 2024

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo ikiwemo Elimu na Afya na kupongeza utekelezaji wa Miradi hasa Shule ya Msingi Malamba inayojengwa kupitia Mfuko wa Elimu.

Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Rehema Liute amesema ubora wa Miradi waliyotembelea inaridhisha huku akisisitiza kasi iongezeke pasipo kuathiri ubora wake.

Kamati hiyo imetembelea Miradi yenye thamani ya Tsh. Milioni 298 ikiwemo Shule ya Msingi Malamba ,
Ujenzi wa matundu 23 ya Vyoo Shule ya Msingi  Mkombozi na Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji Cha mitondi B .

#kaziiendeleešŸ”„

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa