Home » » WILAYA YA SIHA YAFIKA TANDAHIMBA KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI NA MFUKO WA ELIMU.

WILAYA YA SIHA YAFIKA TANDAHIMBA KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI NA MFUKO WA ELIMU.

Agosti 1, 2024

Wataalamu na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Siha kutoka Mkoani Kilimanjaro wamefika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Kwa ajili ya kujifunza namna bora ya ukusanyaji wa Mapato  kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani sambamba na Mfuko wa Elimu ambapo vyote hivyo vinatekelezwa kwa ufanisi katika Wilaya ya Tandahimba.

Awali akizungumza katika Kikao Cha ndani Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Dkt.Christopher Timbuka  amesema wameona ni vema kuja kujifunza Tandahimba Kwa kuwa ni Wilaya inayofanya vizuri kwa ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani .

Katika kipindi Cha Mwaka wa Fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekusanya Mapato kiasi Cha Tsh.Bilioni 6.7 sawa na 120.98% ya Makisio ya Bajeti ambayo ilikuwa Tsh. Bilioni 5.5.
 
Kaziiendelee

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa