Home » » SBL yatoa saruji ya 10m/- kwa waathirika wa tetemeko Kagera

SBL yatoa saruji ya 10m/- kwa waathirika wa tetemeko Kagera

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akimkabidhi  Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu baadhi ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.
Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya makabidhiano ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akifurahi jambo na  Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugul    mara baada ya makabidhiano ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.




Waandishi wa habari wakichukua matukio wakati wa makabidhiano ya msaada wa mifuko ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu akiongea na wafanyakazi wa SBL waliowakilisha katika kutoa msaada wa mifuko ya mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera.Makabidhiano hayo yalifanyika  Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba mapema leo.




Bukoba, Novemba 29, 2016-Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) leo imetoa msaada  mifuko ya saruji 500 yenye thamani ya shilingi milioni 10 kwa wahanga wa janga la tetemeko la ardhi lililotoa mkoani Kagera. Msaada huo ni kuitikia wito wa serikali  kwa mashirika, watu binafsi  na watu wenye mapenzi mema wa kujitoa kusaidia wahanga wa tukio hilo.

Akizungumza katika tukio la kukabidhi msaada huo katika Ofisi ya Mkuuu wa Mkoa wa Kagera mjini Bukoba, Meneja Usalama wa SBL, Sebastian Kalugulu  aliwapa pole  wahanga wa tetemeko hilo  kwa kuwahakikishia kwamba SBL  kila mara iko tayari kusaidia  pindi inapohitajiwa na jamii.

 “”Tunatoa pole ya dhati na masikitiko yetu kwa wahanga wa  tetemeko la ardhi  na tunawaombea majeruhi wote wapone haraka,” alisema Kalugulu, na kuongeza kwamba SBL  inaungana na watu wengine wenye mapenzi mema kutoa msaada wa kibinadamu kwa ajili ya kuwasaidia  kuhimili kadhia iliyowapata  na kurudi katika shughuli zao kawaida.

Kalugulu alithibitisha tena kwamba kampuni hiyo ya bia  imejikita katika kuunga mkono  serikali  na watu binafsi wenye mapenzi mema, mashirika  na makampuni  katika kuisaidia jamii katika maeneo SBL inapoendesha shughuli zake.

 “Ni matumaini yetu kwamba msaada huu utachangia katika michango  iliyokwishatolewa na wasamaria wengine  na kwamba itawawezesha  wahanga hao kujenga  miundombinu iliyoharibika  na hata kuboresha maisha yao.”

 Akizungumzia mchango uliotolewa na SBL, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu alisema kwamba msaada huo unachangia katika michango  mingine  kutoka kwa watu wenye mapenzi mema kutoka ndani, mikoani  na kimataifa  ambao kmwa ukarimu waliitikia wito wa serikali wa kusaidia.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa atahakikisha kuwa  msaada huo unaenda kwenye lengo lililokusudiwa  na kutoa wito  kwa watu zaidi  kuendelea kuwasaidia wahanga.

Mwisho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa