Katika
kutekeleza Malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025, Mamlaka ya
viwanja vya Ndege imedhamiria kufanya maboresho katika Kiwanja cha Ndege
Mtwara kwa kiwango cha Kimataifa ili kuendelea kuimarisha huduma za
usafiri wa anga nchini.
Mapango
huo umeelezwa hivi karibuni na Meneja wa Teknolojia na Mawasiliano
kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini , Bw. Abdulatif Min-Hajj
wakati akitoa taarifa ya maendeleo ya Kiwanja hicho kwa Kaimu Katibu
Mtendaji Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri alipofanya ziara katika
kiwanja hicho ikiwa ni mfululizo wa ziara ya ukaguzi wa miradi ya
maendeleo unaofanywa na timu kutoka Tume ya Mipango.
Meneja
huyo alieleza kuwa mradi huo amabao ni mpango wa muda mrefu unaolenga
katika kufanya upanuzi wa kiwanja pamoja na ujenzi wa jengo la kisasa
kwa ajili ya abiria upo katika hatua za awali ambapo mkandarasi mshauri
tayari amewasilisha rasimu ya taarifa ya mpango mkuu (maste plan).
“Katika
mradi huu kiwanja cha Mtwara kitapanualiwa na kufikia code 4E ambapo
kitakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege kama A340-200. Katika ujenzi wa
jengo la abiria, kwa awamu ya kwanza tutajenga jengo lenye mita za mraba
6570 ili kufikia mahitaji ya mwaka 2023 na awamu ya pili tunatarajia
kuwa na jengo la mita za mraba 10,880 ili kukidhi mahitaji ya abiria kwa
mwaka 2033”, alieleza Meneja huyo.
Kwa
upande wake Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Florence Mwanri
alieleza kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo inasisitiza kuwa na vianzio
mbalimbali vya uchumi na kuwepo kwa miundombinu ya kutosha kuiwezesha
Tanzania kuingia katika nchi za kipato cha kati. Hivyo, mradi huo
utasaidia kuimarisha uchumi wa nchi sambamba na kuongeza ufanisi katika
usafiri wa anga.
Aliongeza kuwa
upanuzi wa kiwanja hicho utakapokamilika sio kwamba tu utasaidia
usafiri wa anga peke yake bali kwa upande mwingine utafungua fursa
mbalimbali za uwekezaji kwa sekta binafsi na kusaidia kuongeza uchumi kwa watanzania.
“Nimeelezwa kuwa mradi huo ukikamilika kutajitokeza fursa za uwekezaji kama kujenga mahoteli makubwa ya hadhi ya nyota tano, kujenga eneo la biashara, ujenzi wa maduka
na migahawa ya kisasa, ujenzi wa visima vya mafuta ya ndege, kutakuwa
na jengo kubwa la kuhifadhia mizigo, na majengo ya kutengenezea ndege.
Hizi zote ni fursa zitakazosaidia kuinua uchumi wa wananchi wetu,”
alieleza.
Hata hivyo Mwanri alishauri kuwa pamoja na kuwa na malengo mazuri ya muda mrefu mamlaka ya hiyo inapaswa kuendelea
kutekeleza malengo yake ya muda mfupi katika kutatua changamoto za
miundombinu ya barabara za ndege kiwanjani hapo ili kuendelea kuimarisha
huduma za usafiri huku akishauri mamlaka hiyo kufanya jitihada za
haraka kupata hati miliki pamoja na kufikiria kujenga uzio katika eneo
la kiwanja hicho.
“Mnapaswa
kuendelea kutekeleza mipango ya muda mfupi wakati mnasubiri mradi
mkubwa utekelezwe. Najua katika bejeti yenu ya sasa mtaendelea
kukarabati miundombinu ili ndege ziendelee kutua na kuondoka kwa
usalama. Vile vile angalieni namna ya kupata hati miliki na kujenga uzio
wa eneo lote kwa ajili ya usalama na kuwadhibiti watu wenye tabia ya
kuvamia maeneo”, Alieleza Mwanri.
0 comments:
Post a Comment