Na Theresia Mwami TEMESA Mtwara.
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu amesema
kuwa hajaridhishwa na ukusanyaji wa mapato na madeni katika kituo cha
Mtwara katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo karakana
imekusanya asilimia 20% tu ya kiasi cha pesa ilichozalisha.
Dkt
Mgwatu amesema kuwa hatovumilia uzembe wowote utakaojitokeza katika
suala la ukusanyaji wa mapato na madeni katika vituo vyote vya TEMESA
nchini.
“Hatuwezi
kuendesha vituo na karakana zetu kwa mwendo huu hivyo inatupasa
kuongeza juhudi katika kufuatilia madeni” alisema Dkt. Mgwatu.
Kwa
upande wake Meneja wa TEMESA Mtwara Mhandisi Said Mongomongo amesema
kuwa kuna changamoto za Taasisi nyingi kutolipa kwa wakati gharama za
matengenezo ya magari na mashine mbalimbali katika karakana yake.
Mhandisi
Mongomongo amewataja baadhi ya wadaiwa sugu kuwa ni pamoja na Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) na Ofisi ya Katibu Tawala mkoani Mtwara.
Akiwa
mkoani Mtwara, Dkt Mgwatu ametembelea Kivuko cha MV. Mafanikio
kinachotoa huduma ya usafiri kati ya Msangamkuu na Msemo pamoja na
Kivuko cha MV. Kilambo kinachotoa huduma kati ya Kilambo (upande wa
Tanzania) na Namoto (upande wa Msumbiji).
Mtendaji
Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Dkt. Mussa Mgwatu yupo
katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Lindi na Mtwara kuangalia
utendaji kazi wa vituo hivyo.
0 comments:
Post a Comment