Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ABIRIA  wanaotumia barabara itokayo Mtwara kwenda Tandahimba na 
Newala wameilalamikia  serikali kwa kushindwa kuitengeneza kwa kiwango 
cha lami licha ya kusafirisha  korosho wakati wa mavuno.
  Akizungumza  na Tanzania Daima, Halima Saidi mkazi  wa Kijiji
 cha Mtama, wilayani Tandahimba, alisema barabara hiyo imekuwa kero  
kwao hata hivyo wanaiomba serikali kuifanyia kazi haraka kwa vile ndiyo 
tegemeo  kwa wakulima wa korosho zao linaloingiza fedha kwenye pato la 
taifa.
  “Barabara  ya Tandahimba-Newala tumesahaulika, hii barabara sio ya 
kuwa na vumbi na  makorongo hadi leo hii wakati serikali inapata fedha 
nyingi kutokana na korosho  kipindi cha msimu kwani hata magari 
yanayosafirisha korosho ni mengi yanalipia  ushuru,” alisema Halima.
  Alisema  ni aibu kwa viongozi wa kusini mpaka leo kuwa kimya bila 
kupigania barabara  zikajengwa kwa lami ili kumsaidia msafiri kufika kwa
 wakati aendako na kuondoa  kero ya usafiri wakati wa mvua.
  “Wilaya  ya Tandahimba ina mapato mengi kupitia korosho lakini haina 
barabara ya lami…  aibu kwa halmashauri tangu nizaliwe miaka 56 
iliyopita nimeikuta barabara ina  vumbi mpaka leo haijawekwa lami.
  “Unasafiri  kutoka Tandahimba ama Newala hadi mtu ufike Mtwara unakuwa
 kama  kinyago kwa sababu ya vumbi… kwanini wasiige Mbeya na 
Kilimanjaro?” alisema  Halima.
  Hassani  Chikota mwanakijiji wa Mkwiti, wilayani humo alisema barabara
 hiyo kwa sasa  inaonekana safi  haina mashimo kwa sababu mwenge wa 
uhuru  umepita ndio maana unaona wamechonga barabara.
 Chanzo:Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment