Home » » ANGALIZO: WIZI WA MITA ZA MAJI WAWA TISHIO MASASI

ANGALIZO: WIZI WA MITA ZA MAJI WAWA TISHIO MASASI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


  Baadhi ya miundombinu ya maji ya Mamlaka (MANAWASA).
MKUU WA WILAYA YA MASASI Hajat FARIDA MGOMI alipokuwa akipanda mti wa kumbukumbu kuzindua mradi wa maji (MANAWASA) MJINI Masasi.
 Na Alvan Limwagu

Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira masasi-Nachingwea (MANAWASA) inatoa masikitiko yake kwa wakazi wa masasi kutokana na matukio yasiyo ya kiustaharabu yanayoendelea hivi sasa ya wizi wa "MITA ZA MAJI" zilizofungwa na wateja kwenye maeneo wanayoishi ambapo mpaka sasa tayari mita 7 zimeshaibiwa na watu wasiojulikana kwenye mitaa ya MKUTI, JIDA pamoja na REST CAMP hivyo Mamlaka ya MANAWASA inawaomba wakazi wote wa mji wa masasi wenye nia njema na huduma hii muhimu kwa wananchi kutoa ushirikiano katika kuwafichua wezi hawa na hatimaye wafikishwe mahakamani kwa hatua nyingine za kisheria. "EWE MKAZI WA MASASI KUMBUKA KWAMBA HAPO AWALI MASASI HAIKUWA HIVI ILIVYO SASA KWENYE SUALA LA MAJI" Hivyo ni vyema kila mmoja akawa mlinzi wa mwenzake ili kuifanya miundombinu ya MANAWASA iendelee kudumu wakati wote... pia MANAWASA inatoa wito kwa wale wenye tabia ya kuchimba mchanga karibu na mabomba ya maji kwenye barabara kuu itokayo mtwara kuingia masasi waache mara moja kwani kwa kufanya hivyo husababisha mabomba hayo kupasuka na maji kushindwa kufika Masasi.

Mtwara yetu Blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa