Home » » KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA DANGOTE

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA DANGOTE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mtaalam kutoka Kampuni Tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) ya GASCO inayojihusisha na usambazaji wa gesi, Mhandisi Mwanaidi Rashid (kulia) akielezea hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa kituo Namba I cha gesi ambapo Kiwanda cha Saruji cha Dangote kitaunganishwa na huduma hiyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwenye ziara hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo ( wa tatu kutoka kulia mbele) na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia ( wa nne kutoka kulia mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na kamati hiyo wakati wa ziara hiyo.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akimpokea Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto) aliyeambatana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti mara baada ya kuwasili katika kiwanda hicho.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (kulia) akielezea mafanikio na changamoto za kiwanda hicho kwa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti (hawapo pichani). Wengine kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, Hawa Ghasia na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Jaji Mstaafu Josephat Mackanja.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo, akifuatilia maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (hayupo pichani ) katika kikao hicho.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (mbele) akielezea jambo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti katika kikao kabla ya kuanza ziara ya kutembelea kiwanda hicho.
Sehemu ya wajumbe kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti na watendaji wa kiwanda cha Dangote wakifuatilia ufafanuzi uliokuwa unatolewa na Mkurugenzi wa Kiwanda cha Uzalishaji wa Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha (hayupo pichani) katika kikao hicho.
Kutoka kulia mbele mtaalam kutoka Idara ya Nishati, Mhandisi Edson Ngabo, Mchumi kutoka Idara ya Sera na Mipango, Josephat Mbwambo na Kaimu Mkurugenzi kutoka Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wakifuatilia maelekezo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge katika kikao hicho.
Mchumi kutoka Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Josephat Mbwambo (kulia) akinukuu hoja mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti katika kikao hicho.
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Jaji Mstaafu Josephat Mackanja akifafanua jambo katika kikao hicho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa