Home » » RC MTWARA AKATAA BARABARA

RC MTWARA AKATAA BARABARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKUU wa Mkoa (RC) wa Mtwara, Kanali mstaafu Joseph SimbakaliaMKUU wa Mkoa (RC) wa Mtwara, Kanali mstaafu Joseph Simbakalia, amekataa kuipokea barabara ya Zambia Mikindani kutokana na kutokamilika kwa wakati.
Kauli hiyo aliitoa mwishoni mwa wiki kwenye kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara Mkoa wa Mtwara mwaka wa fedha 2014/2015, kilichofanyika ukumbi wa Boma mkoani hapa.
Kanali Simbakalia, alisema amewapa siku saba warudi wakamuandalie maelezo upya wakieleza sababu ya barabara hiyo kuchelewa kukamilika kwa muda uliyopangwa.
“Yule mkandarasi miezi mitatu kabla ya kukabidhi barabara, zaidi ya nusu ya vifaa ambavyo vilitakiwa viwepo kwa ajili ya ujenzi havikuwepo na maabara ya ‘ku taste material’ haikuwepo, hiyo si sababu ya msingi ya kuchelewesha barabara, halafu wanasema miundombinu ilikuwa shida…Sasa swali linakuja alifanya hivyo kwa sababu alikuwa hana vifaa hivyo ikiwa na maana wakati anaomba zabuni hakusema ukweli au kafanya makusudi, vifaa anavyo hakuleta, ni kipi kati ya hayo mawili? alihoji Simbakalia na kuongeza:
Taarifa yenu siikubali kuhusiana na barabara hii, hayo unayoniambia muandike kwa sababu maandishi yapo kwa nini tuandikie mate bwana…Andikeni upya maelezo ya kwa nini kumekuwepo na ucheleweshaji kwenye ujenzi wa hiyo barabara, barabara ni muhimu, huu mji mkuu ndio uso wa mkoa wa Mtwara, sasa barabara ilitakiwa ikabidhiwe mwezi wa pili mwaka jana, leo mwezi wa nane 2014, sasa mimi nataka majibu ya uhakika na ya kweli mniletee nione halafu nitaileta taarifa hiyo kwenye kikao kijacho.
Kwa upande wake, Mhandisi wa Manispaa ya Mtwara-Mkindani, Francis Rugemalila, alijitetea kwamba, kuchelewesha kwa barabara ya Zambia Mikindani, alisema kulikuwepo na matatizo ya huo mradi ikiwemo miundombinu na mtaalamu mshauri.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa