Home » » NAHODHA NDANDA AWAPA SOMOWENZAKE

NAHODHA NDANDA AWAPA SOMOWENZAKE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
NAHODHA wa timu iliyopanda Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, Ndanda FC ya mkoani hapa, Salum Hamisi ‘Gallas’, amewataka wachezaji wenzake wasiwe na tabia ya papara kutaka kucheza timu kubwa kama Yanga na Simba, kwani zimekuwa zikiua vipaji vya wachezaji wadogo.
Wito huo ameutoa jana wakati akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu na kubainisha kwamba hawapaswi kubabaika na timu kubwa, kwa sababu leo wakitoka Ndanda kwenda Yanga ama Simba, watasajiliwa vizuri, lakini itakuwa ngumu kupata nafasi ya kucheza na kuonekana zaidi.
“Tusiwe na papara na wala tusidanganyike kwa sababu tu ni klabu kubwa, lakini zinatumaliza sisi wachezaji wadogo, kwa sababu leo ukitoka hapa kwenye timu yako ya Ndanda kwenda Yanga au Simba, umesajiliwa vizuri, lakini huwezi kupata nafasi ya kucheza ili uonekane zaidi, sana sana watakuwa wanakiua kipaji chako cha uchezaji, kwani unapokaa bila kucheza kwa muda mrefu na kipaji kinapotea,” alisema Gallas.
Pamoja na mambo mengine, Gallas alisema kuwa kitu ambacho wamekifanya hadi kupata mafaniko ya kupanda daraja ni kujituma na uvumilivu ndani ya timu yao.
“Kitu kikubwa ambacho kimetufanya hadi kupata mafanikio ya kupanda daraja, ni kujituma na uvumilivu ndani ya timu na kuwasikiliza viongozi wetu walivyokuwa wanatuambia, hiyo ndio siri kubwa ya mafanikio yetu,” alisema.
Nahodha huyo aliwaomba wapenzi na mashabiki wa Ndanda FC, wasiache hamasa ambayo wameifanya kwa kuwashangilia na kuwafuata kila walipokuwa wanacheza, bali waendelee nayo kwani imewahamasisha na kufanya vizuri.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa