Home » » Bei mpya ya korosho yatangazwa

Bei mpya ya korosho yatangazwa



Mtwara

MKUTANO mkuu wa mwaka wa wadau wa tasnia ya korosho nchini umeamua na kutangaza bei dira ya zao la korosho msimu wa 2013/2014 kuwa shs 1000 kwa kilo daraja la kwanza na shs 800 kwa daraja pili.

Uamuzi huo umefikiwa baada ya mvutano mkubwa wa wajumbe pale wajumbe walipotofautiana na bei dira iliyokuwa imependekezwa na bodi ya korosho nchini ya shs. 800 kwa kilo daraja la kwanza na shs 600 kwa kilo daraja la pili.

Kufuatia uamuzi huo bei hiyo ndiyo bei anzia na bei inaweza kuongezeka kutegemeana na hali ya soko katika mnada wa zao hilo.

Aidha mkutano umeelekeza mfumo wa stakabadhi ghalani ili ufanikiwe kusiwepo vibali vya kununua korosho tofauti na mfumo wa stakabadhi ghalani kufanikisha na kuwepo ukaguzi wa mkaguzi mkuu wa serikali pale inapobainika upotevu wa fedha.

Mkutano huo uliojumuisha wajumbe zaidi ya 700 kutoka wilaya zote 44 zinazolima zao la korosho nchini ulikuwa unachambua changamoto mablimbali na kuweka mstakabali wa zao la korosho nchini.

Zaidi ya tani 141,000 za korosho msimu uliopita wa 2012/2013 ambapo zaidi ya asilimia 80 ya korosho zote zimeuzwa nje nchi zikiwa ghafi.





0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa