Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kaimu
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Elias Nyabusami akifungua mafunzo
yaWaganga Wakuu, Makatibu wa Afya,Maafisa TEHAMA,Maafisa
Mipango,Wahasibu na Wachumi kutoka katika Mikoa ya Lindi,Mtwara, Ruvuma
na Dar es Salaam kuhusu mfumo mpya wa kuandaa Mipango na bajeti za
Mamlaka ya Serikali za Mitaa leo mjini Mtwara.
Mkuu
wa Timu ya Rasilimali Fedha Kutoka mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya
Sekta za Umma ujulikanao kwa Kiingereza kama (Public Sector Systems
Streghthen PS3.) unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la
Marekani (USAID) Bw. Gemini Mtei akizungumza wakati wa mafunzo hayo leo
Mjini Mtwara.
Afisa
TEHAMA mwandamizi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI bw. Archibold Kundasai
akitoa maelezo kwa washiriki kuhusu faida za mfumo wa PS3 wakati wa
hafla yaufunguzi wa mafunzo hayo.
Mmoja wa watoa mada kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI bw. James Mtakatifikolo akiwasilisha mada katika mafunzo hayo.
Washiriki wa Mafunzo hayo wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasiishwa.
Kaimu
Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bw. Elias Nyabusami (Katikati) akiwa
na sehemu ya washiriki wa mafunzo hayo kwenye picha ya pamoja mara
baada ya kufungua mafunzo hayo.
Meneja
wa mradimradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ujulikanao kwa
Kiingereza kama (Public Sector Systems Streghthen PS3.) Mkoa wa Mtwara
unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID)
Bw. Deosdedit Msofe akizungumza wakati wa mafunzo hayo leo Mjini Mtwara.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo akizungumza wakati wa mafunzo hayo leo mjini Mtwara.
(Picha zote na Frank Mvungi- Maelezo Mtwara)
Frank Mvungi Maelezo
Serikali
kuokoa Kiwango Kikubwa cha Fedha kutokana na kuanza kutumika kwa mfumo
ulioboreshwa katika kuandaa Mipango na Bajeti za Mamlaka ya Serikali za
Mitaa uitwao Plan Rep unaoenda sambamba na mafunzo yanayoendeshwa
kupitia mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ujulikanao kwa
Kiingereza kama (Public Sector Systems Streghthen PS3.) unaofadhiliwa na
Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Marekani (USAID).
Akifungua
mafunzo kwa yaliyowashirikisha Waganga Wakuu, Makatibu wa Afya,Maafisa
TEHAMA,Maafisa Mipango,Wahasibu,Wachumi kutoka katika Mikoa ya
Lindi,Mtwara, Ruvuma na Dar es Salaam ,Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa
Mtwara Bw.Elias Nyabusami amesema mafunzo hayo yamekuja wakati muafaka
na yatasaidia kuondoa Changamoto zilizokuwa zikijitokeza kabla ya kuwepo
kwa mfumo huo.
‘’Kutokana
na mabadiliko na kurahisishwa kwa Teknolojia mfumo mpya wa Plan Rep
umerahisihwa kwa kufanywa kuwa web Based na utawezesha Halmashauri
kuingiza taarifa za mipango na bajeti moja kwa moja kwa njia ya mtandao
na kuweza kutumwa kwenye mfumo mmoja uliopo Ofisi ya Rais TAMISEMI ili
kufanyiwa kazi na kuingizwa kwenye bajeti Kuu ya mwaka
husika”Alisisitiza Nyabusami
Akifafanua
amesema kuwa mfumo huo utasaidia kutoa mrejesho wa mara kwa mara kwa
ngazi husika za utawala kwa wakati na hakutakuwa tena na haja ya
wahusika kusafiri kutoka katika vituo vyao vya kazi ili kushughulikia
masuala ya bajeti na Mipango kwa kuwa sasa yatafanyika katika Mikoa na
Halmashauri husika.
Kwa
upande wake Mkuu wa Timu ya Rasilimali Fedha Kutoka mradi wa
Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma ujulikanao kwa Kiingereza kama
(Public Sector Systems Streghthen PS3.) Bw. Germini Mtei amesema kuwa
kupitia mfumo mpya wa Plan Rep Mipango yote na Bajeti za Vituo vya
kutolea Huduma kwa wananchi itaonekana kupitia mfumo huo hali
itakayosaidia kuongeza ufanisi,uwazi , uwajibikaji na kuboreshwa kwa
utoaji huduma.
“Kwa
kutumia mfumo huu mpya sasa tunaamini kuwa utasaidia kuondoa
ucheleweshaji wa fedha kwenda kwenye miradi na upotevu wa fedha kwa kuwa
kila kitu kitafanyika kwa njia ya mtandao” Alisisitiza Mtei.
Aliongeza
kuwa mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya sekta za Umma (PS3)
unaotekelezwa katika mikoa 13 na Halmashauri 93 za Tanzania bara na PS3
inafanya kazi katika sekta mbalimbali ikiwemo kuimarisha mifumo ya
mawasiliano,Utawala Bora,Fedha na rasilimali watu,husasani kwa jamii
zenye uhitaji.
Aidha
Afisa TEHAMA mwandamizi toka Ofis ya Rais TAMISEMI Bw. Archibold
Kundasai amesema kuwa mipango yote kuanzia ngazi ya Kata,Halmashauri na
Mikoa itakuwa katika mfumo huo na dhamira ya Serikali ni kuongeza tija
katika kuwahudumia Wananchi.
“Bajeti
ilikuwa ikichukua muda mrefu kuandaliwa ambapo takribani miezi 4
ilitumika ambapo kwa mfumo huu tija itaongezeka kwa kuwa wahusika
watabaki katika vituo vyao wakihudumia wananchi huku wakitekeleza jukumu
la Kuandaa Bajeti na Mipango yao” Alisisitiza Kundasai
Naye
Mshiriki wa Mafunzo hayo Bw. Ezekiel Buyagaza ambaye ni Afisa Mipango
wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi amesema kuwa anaipongeza Serikali
kwa maboresho yanayofanyika hali itakayochochea tija katika kutoa huduma
kwa wananchi.
Serikali
ya Tanzania na USAID kupitia mradi wa uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za
Umma (PS3)imeandaa mafunzo haya kwa watumiaji wake nchi nzima,Mafunzo
yanatolewa na Wakufunzi kutoka Ofisi ya Rais TAMISEMI,Wakala ya Serikali
mtandao,Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora,Wizara ya Fedha na
Mipango,Wizara ya afya na unatarajiwa kutumiwa na watumiaji 1500
watakaofundishwa matumizi ya mfumo huo.
0 comments:
Post a Comment