Home » » Shule za msingi zasaidiwa vitabu

Shule za msingi zasaidiwa vitabu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Shule zilizonufaika na msaada huo ni pamoja na shule ya msingi Mangaka, Nahawara, Ndwika 2 na Mtokora ambazo zote ni kutoka katika kata ya Mangaka, Halmashauri ya Wilaya ya Nanyumbu mkoani Mtwara. Vitabu alivyonunua diwani huyo ni 388 vya Sayansi na 100 vya Stadi za Kazi.
Pia alinunua makasha manne ya kalamu ambazo watapewa walimu wa shule za msingi katika kata hiyo.
Akizungumza jana wakati wa kukabidhi msaada huo kwa walimu wakuu wa shule hizo katika viwanja vya shule ya msingi Mangaka, alisema ameamua kununua vitabu vingi vya Sayansi kutokana na ugunduzi wa gesi mkoani humo ambao wengi wa wataalamu wanaohitajika ni wale waliosoma masomo ya Sayansi.
Alisema kutokana na kero ya upungufu wa vitabu kwenye kata hiyo waliyokuwa wanailalamikia walimu, ndicho kilichomsukuma kuamua kununua vitabu hivyo ambapo kwa sasa kila mtoto wa darasa la nne atatumia kitabu kimoja kama inavyotakiwa kitaalamu.
Mchoma alisema kwa vitabu vya awamu ya kwanza alivyonunua vina thamani ya Sh milioni 1.1. Lengo lake kwa sasa ni kutatua changamoto zilizopo kwenye shule hizo ikiwemo upungufu wa madawati, matundu ya vyoo,vyumba vya madarasa pamoja na nyumba za walimu.
“Nimeguswa na tatizo la wanafunzi wa kata yangu kutumia kitabu kimoja zaidi ya wanafunzi wawili, ndio maana nimeamua kununua vitabu hivi ambavyo kwa sasa naamini kila mwanafunzi anayesoma darasa la nne kwenye kata hii atatumia kitabu chake na nitafanya hivi kwa kipindi chote cha uongozi wangu ndani ya miaka mitano,”alisema Mchoma.
Ofisa Elimu taaluma wa shule za msingi wilayani Nanyumbu, Stephen Urassa alimpongeza diwani huyo kwa namna alivyoonesha njia .
Mratibu elimu wa kata ya Mangaka, Fidelis Hokororo alisema kata hiyo ina jumla ya wanafunzi 253 wa darasa la nne ambao kutokana na msaada huo, kwa sasa kila mwanafunzi wa darasa la nne atakuwa anatumia kitabu kimoja cha sayansi.

Chanzo Gazeti la Habari leo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa