
Halmashauri ya Mji Nanyamba inatarajia kutekeleza mradi wa ujenzi wa shule ya ufundi stadi itakayojengwa katika mtaa wa Nanyamba B Kata ya Nanyamba kwa ufadhili wa SEQUIP.Taarifa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango iliyowasilishwa Leo tarehe 31/07/2024 katika Baraza la Madiwani ilieleza kuwa tayari Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Nanyamba (WDC) imefanikiwa kulipa fidia na kutwaa eneo lenye ukubwa ekari 10 kwa gharama ya shilingi 20,000,000 (Milioni ishirini) inayotokana na michango ya shilingi ishirini iliyokatwa kwa wakulima wa korosho.“Itakuwa ni shule kubwa ambayo itakuwa na mabweni, karakana, maabara na itakusanya wanafunzi wa Halmashauri...