KAMATI YA FEDHA TANDAHIMBA YARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO
Agosti 5, 2024
Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo ikiwemo Elimu na Afya na kupongeza utekelezaji wa Miradi hasa Shule ya Msingi Malamba inayojengwa kupitia Mfuko wa Elimu.
Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Rehema Liute amesema ubora wa Miradi waliyotembelea inaridhisha huku akisisitiza kasi iongezeke pasipo kuathiri ubora wake.
Kamati hiyo imetembelea Miradi yenye thamani ya Tsh. Milioni 298 ikiwemo Shule ya Msingi Malamba ,
Ujenzi wa matundu 23 ya Vyoo Shule ya Msingi Mkombozi na Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji Cha mitondi B .
#kaziiendeleeš„
Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo ikiwemo Elimu na Afya na kupongeza utekelezaji wa Miradi hasa Shule ya Msingi Malamba inayojengwa kupitia Mfuko wa Elimu.
Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Rehema Liute amesema ubora wa Miradi waliyotembelea inaridhisha huku akisisitiza kasi iongezeke pasipo kuathiri ubora wake.
Kamati hiyo imetembelea Miradi yenye thamani ya Tsh. Milioni 298 ikiwemo Shule ya Msingi Malamba ,
Ujenzi wa matundu 23 ya Vyoo Shule ya Msingi Mkombozi na Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji Cha mitondi B .
#kaziiendeleeš„
MRADI WA CHUMBA CHA KOMPYUTA WAZINDURIWA LUAGALA SEKONDARI.
Mwenyekiti wa Mfuko wa Elimu Wilaya ya Tandahimba Mshamu Bakiri amezindua Mradi wa Chumba Cha Kompyuta Shule ya Sekondari Luagala Kwa ajili ya wanafunzi wa Shule hiyo kuweza kujifunza Masomo yao pamoja na kuwa na Ujuzi wa TEHAMA.
Mradi wenye Gharama ya Tsh.Milioni 70 ukijumuisha Chumba Cha kompyuta, Meza na Kompyuta 25 umefadhiliwa na Taasisi ya CAMARA EDUCATION TANZANIA ambayo imelenga kurahisisha ufundishaji na ujifunzaji, kuongeza Ujuzi wa matumizi ya Kompyuta na TEHAMA na hatimaye kuzalisha wataalamu wenye Ujuzi wa TEHAMA hapo baadae.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Francis Mkuti amewaasa Wanafunzi akisema
" Mkiitumia Vizuri ufaulu utaongezeka na tunawadai matokeo,hatutarajii kupata Sifuri kwa kuwa Mazingira yameboreshwa"
Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo DCI.Mariam Mwanzalima amewashukuru wafadhili hao kuwa sehemu ya kuboresha Miundombinu ya Sekta ya Elimu akisisitiza Wanafunzi kutumia Kompyuta hizo kwa matumizi yaliyokusudiwa.
Katika Uzinduzi huo Viongozi mbalimbali wamehudhuria akiwemo Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya, baadhi ya Madiwani na Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Elimu .
#kaziiendelee
Mradi wenye Gharama ya Tsh.Milioni 70 ukijumuisha Chumba Cha kompyuta, Meza na Kompyuta 25 umefadhiliwa na Taasisi ya CAMARA EDUCATION TANZANIA ambayo imelenga kurahisisha ufundishaji na ujifunzaji, kuongeza Ujuzi wa matumizi ya Kompyuta na TEHAMA na hatimaye kuzalisha wataalamu wenye Ujuzi wa TEHAMA hapo baadae.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Francis Mkuti amewaasa Wanafunzi akisema
" Mkiitumia Vizuri ufaulu utaongezeka na tunawadai matokeo,hatutarajii kupata Sifuri kwa kuwa Mazingira yameboreshwa"
Kwa Upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo DCI.Mariam Mwanzalima amewashukuru wafadhili hao kuwa sehemu ya kuboresha Miundombinu ya Sekta ya Elimu akisisitiza Wanafunzi kutumia Kompyuta hizo kwa matumizi yaliyokusudiwa.
Katika Uzinduzi huo Viongozi mbalimbali wamehudhuria akiwemo Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya, baadhi ya Madiwani na Wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Elimu .
#kaziiendelee
WILAYA YA SIHA YAFIKA TANDAHIMBA KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI NA MFUKO WA ELIMU.
Agosti 1, 2024
Wataalamu na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Siha kutoka Mkoani Kilimanjaro wamefika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Kwa ajili ya kujifunza namna bora ya ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani sambamba na Mfuko wa Elimu ambapo vyote hivyo vinatekelezwa kwa ufanisi katika Wilaya ya Tandahimba.
Awali akizungumza katika Kikao Cha ndani Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Dkt.Christopher Timbuka amesema wameona ni vema kuja kujifunza Tandahimba Kwa kuwa ni Wilaya inayofanya vizuri kwa ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani .
Katika kipindi Cha Mwaka wa Fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekusanya Mapato kiasi Cha Tsh.Bilioni 6.7 sawa na 120.98% ya Makisio ya Bajeti ambayo ilikuwa Tsh. Bilioni 5.5.
Wataalamu na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Siha kutoka Mkoani Kilimanjaro wamefika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Kwa ajili ya kujifunza namna bora ya ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani sambamba na Mfuko wa Elimu ambapo vyote hivyo vinatekelezwa kwa ufanisi katika Wilaya ya Tandahimba.
Awali akizungumza katika Kikao Cha ndani Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Dkt.Christopher Timbuka amesema wameona ni vema kuja kujifunza Tandahimba Kwa kuwa ni Wilaya inayofanya vizuri kwa ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani .
Katika kipindi Cha Mwaka wa Fedha 2023/2024 Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekusanya Mapato kiasi Cha Tsh.Bilioni 6.7 sawa na 120.98% ya Makisio ya Bajeti ambayo ilikuwa Tsh. Bilioni 5.5.
Kaziiendelee
KATA YA DINYECHA YAOMBA VIJIJI VIWILI KUPEWA HADHI YA MITAA
Ikiwa
ni mkutano wa mwisho wa Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2023/2024
kupokea na kujadili taarifa za Maendeleo za kata kwa robo ya nne, Leo
tarehe 30/07/2024 Kata ya Dinyecha imewasilisha ombi la vijiji viwili
Chikwaya na Kibaoni kupewa hadhi ya mitaa. Kwa sasa kata ya Dinyecha Ina
Vijiji viwili, Mitaa mitatu na Vitongoji 11.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Nanyamba, Eng. Mshamu A. Munde aliahidi kutuma timu ya wataalamu kuangalia ikiwa vijiji hivyo vina sifa ya kuwa mitaa kabla ya kupeleka ombi hilo ngazi za juu kwaajili ya mchakato zaidi.
Akitoa maoni kuhusu taarifa za maendeleo za kata zilizowasilishwa Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, Mhe. Abdallah Dadi Chikota aliwataka wajumbe kuonesha miradi ya maendeleo zinazotekelezwa katika kata zao bila kujali chanzo cha fedha au taasisi wezeshi.
“Mfano kata ya Kitaya kuna mradi mkubwa wa maji utakaotoa maji kijiji cha Maembejuu kwenda Mchanje mpaka kijiji cha Maembechini ambao tayari umefikia 80% lakini kwenye taarifa haijaoneshwa. Hata kule kata ya Nyundo kuna ujenzi wa Zahanati na kijiji cha Niyumba pamoja na ujenzi wa shule fedha za BOOST taarifa haijaainisha hayo.”Alisema Mhe. Chikota
Katika hatua nyingine Mkurugenzi amewataka watendaji wa kata kuhakikisha makusanyo katika kata zako hayashuki 80% kwa ustawi mzuri wa Halmashauri.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Nanyamba, Eng. Mshamu A. Munde aliahidi kutuma timu ya wataalamu kuangalia ikiwa vijiji hivyo vina sifa ya kuwa mitaa kabla ya kupeleka ombi hilo ngazi za juu kwaajili ya mchakato zaidi.
Akitoa maoni kuhusu taarifa za maendeleo za kata zilizowasilishwa Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, Mhe. Abdallah Dadi Chikota aliwataka wajumbe kuonesha miradi ya maendeleo zinazotekelezwa katika kata zao bila kujali chanzo cha fedha au taasisi wezeshi.
“Mfano kata ya Kitaya kuna mradi mkubwa wa maji utakaotoa maji kijiji cha Maembejuu kwenda Mchanje mpaka kijiji cha Maembechini ambao tayari umefikia 80% lakini kwenye taarifa haijaoneshwa. Hata kule kata ya Nyundo kuna ujenzi wa Zahanati na kijiji cha Niyumba pamoja na ujenzi wa shule fedha za BOOST taarifa haijaainisha hayo.”Alisema Mhe. Chikota
Katika hatua nyingine Mkurugenzi amewataka watendaji wa kata kuhakikisha makusanyo katika kata zako hayashuki 80% kwa ustawi mzuri wa Halmashauri.

HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA KUJENGA SHULE KUBWA YA UFUNDI.
Halmashauri ya Mji Nanyamba inatarajia kutekeleza mradi wa ujenzi wa shule ya ufundi stadi itakayojengwa katika mtaa wa Nanyamba B Kata ya Nanyamba kwa ufadhili wa SEQUIP.
Taarifa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango iliyowasilishwa Leo tarehe 31/07/2024 katika Baraza la Madiwani ilieleza kuwa tayari Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Nanyamba (WDC) imefanikiwa kulipa fidia na kutwaa eneo lenye ukubwa ekari 10 kwa gharama ya shilingi 20,000,000 (Milioni ishirini) inayotokana na michango ya shilingi ishirini iliyokatwa kwa wakulima wa korosho.
“Itakuwa ni shule kubwa ambayo itakuwa na mabweni, karakana, maabara na itakusanya wanafunzi wa Halmashauri yote. Mwanafunzi akihitimu pale kutakuwa na cheti cha taaluma pamoja na cheti cha ufundi.” Alieleza Mhe. Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba.
Katika hatua nyingine madiwani wamepiga kura za kumchagua Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, ambapo Mhe. Maliki Hamis Majali, Diwani wa kata ya Kiromba amepigiwa kura za Ndio kuendelea na nafasi yake hiyo.
Aidha, Mhe. Jamal Abdallah Kapende, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nanyamba ametangaza kamati mpya za kudumu zitakazoanza kazi kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Taarifa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango iliyowasilishwa Leo tarehe 31/07/2024 katika Baraza la Madiwani ilieleza kuwa tayari Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Nanyamba (WDC) imefanikiwa kulipa fidia na kutwaa eneo lenye ukubwa ekari 10 kwa gharama ya shilingi 20,000,000 (Milioni ishirini) inayotokana na michango ya shilingi ishirini iliyokatwa kwa wakulima wa korosho.
“Itakuwa ni shule kubwa ambayo itakuwa na mabweni, karakana, maabara na itakusanya wanafunzi wa Halmashauri yote. Mwanafunzi akihitimu pale kutakuwa na cheti cha taaluma pamoja na cheti cha ufundi.” Alieleza Mhe. Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba.
Katika hatua nyingine madiwani wamepiga kura za kumchagua Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri, ambapo Mhe. Maliki Hamis Majali, Diwani wa kata ya Kiromba amepigiwa kura za Ndio kuendelea na nafasi yake hiyo.
Aidha, Mhe. Jamal Abdallah Kapende, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Nanyamba ametangaza kamati mpya za kudumu zitakazoanza kazi kwa mwaka wa fedha 2024/2025.