TUSOME MAGAZETI YA LEO KUTOKA MKOA WA MTWARA

Magazeti                 &nb...

KAMATI YA FEDHA TANDAHIMBA YARIDHISHWA NA MIRADI YA MAENDELEO

Agosti 5, 2024Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba imekagua Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo ikiwemo Elimu na Afya na kupongeza utekelezaji wa Miradi hasa Shule ya Msingi Malamba inayojengwa kupitia Mfuko wa Elimu.Akizungumza wakati wa Ziara hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Rehema Liute amesema ubora wa Miradi waliyotembelea inaridhisha huku akisisitiza kasi iongezeke pasipo kuathiri ubora wake.Kamati hiyo imetembelea Miradi yenye thamani ya Tsh. Milioni 298 ikiwemo Shule ya Msingi Malamba , Ujenzi wa matundu 23 ya Vyoo Shule ya Msingi  Mkombozi na Ujenzi wa Zahanati ya Kijiji...

MRADI WA CHUMBA CHA KOMPYUTA WAZINDURIWA LUAGALA SEKONDARI.

Mwenyekiti wa Mfuko wa Elimu Wilaya ya Tandahimba Mshamu Bakiri amezindua Mradi wa  Chumba Cha Kompyuta Shule ya Sekondari Luagala  Kwa ajili ya wanafunzi wa Shule hiyo kuweza kujifunza Masomo yao pamoja na kuwa na Ujuzi wa TEHAMA.Mradi wenye Gharama ya Tsh.Milioni 70 ukijumuisha Chumba Cha kompyuta, Meza na Kompyuta 25 umefadhiliwa na Taasisi ya CAMARA EDUCATION TANZANIA ambayo imelenga kurahisisha ufundishaji na  ujifunzaji, kuongeza Ujuzi wa matumizi ya Kompyuta na TEHAMA na hatimaye kuzalisha wataalamu wenye Ujuzi wa TEHAMA hapo baadae.Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba Francis Mkuti amewaasa Wanafunzi akisema" Mkiitumia...

WILAYA YA SIHA YAFIKA TANDAHIMBA KUJIFUNZA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI NA MFUKO WA ELIMU.

Agosti 1, 2024Wataalamu na Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Siha kutoka Mkoani Kilimanjaro wamefika Halmashauri ya Wilaya ya Tandahimba Kwa ajili ya kujifunza namna bora ya ukusanyaji wa Mapato  kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani sambamba na Mfuko wa Elimu ambapo vyote hivyo vinatekelezwa kwa ufanisi katika Wilaya ya Tandahimba.Awali akizungumza katika Kikao Cha ndani Mkuu wa Wilaya ya Siha Mhe.Dkt.Christopher Timbuka  amesema wameona ni vema kuja kujifunza Tandahimba Kwa kuwa ni Wilaya inayofanya vizuri kwa ukusanyaji wa Mapato kupitia Mfumo wa Stakabadhi ghalani .Katika kipindi Cha Mwaka wa Fedha 2023/2024 Halmashauri...

KATA YA DINYECHA YAOMBA VIJIJI VIWILI KUPEWA HADHI YA MITAA

Ikiwa ni mkutano wa mwisho wa Baraza la Madiwani kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kupokea  na kujadili taarifa za Maendeleo za kata kwa robo ya nne, Leo tarehe 30/07/2024 Kata ya Dinyecha imewasilisha ombi la vijiji viwili Chikwaya na Kibaoni kupewa hadhi ya mitaa. Kwa sasa kata ya Dinyecha Ina Vijiji viwili, Mitaa mitatu na Vitongoji 11.Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Nanyamba, Eng. Mshamu A. Munde aliahidi kutuma timu ya wataalamu kuangalia ikiwa vijiji hivyo vina sifa ya kuwa mitaa kabla ya kupeleka ombi hilo ngazi za juu kwaajili ya mchakato zaidi.Akitoa maoni kuhusu taarifa za maendeleo za kata zilizowasilishwa Mbunge wa Jimbo...

HALMASHAURI YA MJI NANYAMBA KUJENGA SHULE KUBWA YA UFUNDI.

Halmashauri ya Mji Nanyamba inatarajia kutekeleza mradi wa ujenzi wa shule ya ufundi stadi itakayojengwa katika mtaa wa Nanyamba B Kata ya Nanyamba kwa ufadhili wa SEQUIP.Taarifa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango iliyowasilishwa Leo tarehe 31/07/2024 katika Baraza la Madiwani ilieleza kuwa tayari Kamati ya Maendeleo ya Kata ya Nanyamba (WDC) imefanikiwa kulipa fidia na kutwaa eneo lenye ukubwa ekari 10 kwa gharama ya shilingi 20,000,000 (Milioni ishirini) inayotokana na michango ya shilingi ishirini iliyokatwa kwa wakulima wa korosho.“Itakuwa ni shule kubwa ambayo itakuwa na mabweni, karakana, maabara na itakusanya wanafunzi wa Halmashauri...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa