Home » » Bodaboda waandamana Mtwara

Bodaboda waandamana Mtwara

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Madereva pikipiki maarufu kama bodaboda mkoani hapa, wameandamana hadi Kituo Kikuu cha Polisi wakipinga hatua ya polisi kuwakamata na kuwapiga.
Maandamano hayo yalisababisha shughuli mbalimbali kusimama baada ya polisi kuingilia kati na kuyatuliza kwa vile hayakupata kibali.
Hofu miongoni mwa wananchi ilikuwa kubwa kutokana na polisi kutanda sehemu mbalimbali.
Mashuhuda walisema kuwa polisi walalizimika kuingilia kati ili kuwatawanya madereva hao wa bodaboda na kuleta hofu kubwa.
Madereva hao wanadai kuwa askari wa usalama barabarani wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwakamata na kuwapiga bila sababu za msingi. Mmoja kati ya madereva hao ambaye hakutaka jina lake kuandikwa kwenye gazeti, alisema walikaa kikao na polisi na kuafikiana kila dereva kuwa na kofia ya kuvaa kichwani pamoja na abiria atakayembeba.
“Tulikubaliana baada ya miezi mitatu kila dereva lazima awe na kofia ya usalama kuvaa kichwani,” alisema.
“Tumeshangazwa na hatua ya polisi kuanza kutukamata kabla hata ya muda tuliokubaliana kufika.”
Alisema pamoja na kujitetea, polisi wamekuwa wakiwakamata, wakitupiga na kutulazimisha kuwaambia abiria wanaowabeba kuvaa kofia.
Aliongeza: “Abiria hawataki kuvaa kofia kwa madai wanaogopa kuambukizwa ugonjwa wa ngozi, na sisi hatuwezi kuwalazimisha.
“Hatuna uhakika na madai ya abiria kukataa kuvaa kofia kwa kuhofia kuambukizwa magonjwa ya ngozi. ”
Alipoulizwa Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, Zelothe Stephen kuhusu maandamano hayo, alimtaka mwandishi kuandika malalamiko ya madereva hao na kwamba angeyajibu baadaye.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa