Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya sekondari ya Mtwara
Ufundi mkoani Mtwara, Tawfiq Hamisi (17), amefariki dunia baada ya
kukatwa na kiwembe katika mkono wake wa kulia na mwanafunzi mwenzake
Issac Yohana (16)
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, kamanda wa polisi mkoa wa
Mtwara, Henry Mwaibambe, amesema kabla ya kifo hicho kulikuwa na ugonvi
kati ya marehemu na mtuhumiwa ambaye ni Isaac anayedaiwa kuficha kiatu
cha mwenzie ambapo baada ya mzozano akaamua kumkata na kiwembe mwenzie
chini ya bega lake la kulia.
Ameongeza kuwa marehemu ni mwenyeji wa mkoa wa Tanga huku mtuhumiwa
ni mwenyeji wa wiayani Newala mkoani Mtwara, na kwamba taratibu za
kuusafirisha mwili wa marehemu kuupeleka kwao zinafanywa na uongozi wa
shule, huku mtuhumiwa akishikiliwa na jeshi la polisi kwa upelelezi
zaidi.
Mganga mfawidhi wa hospitali ya Ligula, Dkt. Mdoe Mhuza,
amethibitisha kupokelewa kwa mwili wa marehemu majira ya saa 11 alfajiri
na kudai kuwa bado uchunguzi zaidi unaendelea kwa ajili ya kuweza
kubaini chanzo cha kifo chake.
0 comments:
Post a Comment