Home » » Kampuni ya Tigo yakabidhi madawati manispaa ya Mtwara leo

Kampuni ya Tigo yakabidhi madawati manispaa ya Mtwara leo



Mkuu wa wilaya ya Mtwara Dkt. Khatibu Kazungu (kulia)akipokea moja kati ya madawati 135 yenye thamani ya shilingi milioni 22/- kwa mkoa wa Mtwara toka kwa Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles kwenye makabidhiano yaliyofanyika shule ya msingi Maendeleo, manispaa ya Mtwara leo.



Mkuu wa wilaya ya Mtwara Dkt. Khatibu Kazungu (kulia)akiwa ameketi na mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani Goodluck Charles mara baada ya makabidhiano ya madawati 135 kwa manispaa ya mkoa wa Mtwara . Hafla iliyofanyika  shule ya msingi Maendeleo leo,



Mkuu wa wilaya ya Mtwara Dkt. Khatibu Kazungu (kulia) na mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani Goodluck Charles, wanafunzi wa shule ya msingi maendeleo, Hajira Shaibu (wa pili kulia), Ezra  Joseph na mwalimu wao Fabiola Haule(kushoto) wakiwa wameketi mara baada makabidhiano ya madawati 135 kwa manispaa ya Mtwara leo



Mkuu wa wilaya ya Mtwara Dkt Khatibu Kazungu na mkurugenzi wa Tigo kanda ya pwani Goodluck Charles wakiwa wamepozi na viongozi mbalimbali wa manispaa ya wilaya ya Mtwara Mikindani kwenye hafla ya makabidhiano ya madawati leo.



Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Maendeleo manispaa ya Mtwara, Fabiola Haule akitoa neno la shukrani kwa kampuni ya simu za mkononi ya Tigo leo, mara baada ya kupokea madawati.


Wanafunzi wakifurahia 


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa