Home » » Usaili wa Maisha Plus Mtwara, funga kazi

Usaili wa Maisha Plus Mtwara, funga kazi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Ni asubuhi tulivu katika fukwe za bahari ya hindi kusini mwa Tanzania ambapo vijana wengi wamejitokeza kufanya usaili wa mashindano ya Maisha Plus East Africa 2016. Wapo wanaoonekana kujiamini na wengine wamejawa uoga. "Ni siku niliyoisubiri kwa hamu sana" anasema Faustine Komba miongoni mwa washiriki kutoka Mtwara.
678A0009
Safari ya msimu wa tano wa mashindano ya Maisha Plus imeanza rasmi kwa kuanza na usaili uliofanyika katika hotel ya NAF Beach iliyoko Mtwara. Washiriki kutoka mikoa ya jirani nao pia walijitokeza. "Maisha Plus kwangu ni ndoto ya muda mrefu sana, niliposikia mnakuja Mtwara nikasema piga ua lazima nishiriki" Anasema Ismail Likando aliyesafiri kutoka Lindi.
678A0022
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9916
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9925
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Maswali mengi yalilenga kupima uelewa wa vijana kuhusu mambo mbalimbali ya kijamii ikiwemo mtazamo wao juu ya mwenendo wa kiuchumi. Mengine yalilenga kuwachanganya tu.
678A9961
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A9971
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Mshiriki Grace Pemba anaelezea changamoto mbalimbali alizokutana nazo kutokana na kuolewa akiwa na umri mdogo, anasema hadi sasa ana watoto wawili ambao wanaishi na baba yao. Alipoulizwa maswali zaidi Grace alijawa na simanzi na kujikuta akitoa machozi, "Nimelia kwa sababu mmenikumbusha nyuma nilikotokea" anasema Grace mfanyakazi wa Saloon kutoka mkoani Mtwara.
A video posted by Maisha Plus (@maishaplus2016) on Jun 4, 2016 at 6:47am PDT
678A9980
Mshiriki Grace Pemba akijifuta machozi.
Wakati usaili ukiendelea hali ya kujaa kwa maji baharini ilitokea na kulazimisha timu ya Maisha Plus kubadili utaratibu wa awali wa upigaji picha.
678A0075
Waandaaji wa mashindano ya Maisha Plus wakibadili utaratibu wa awali wa kupiga picha baada ya maji kujaa.
678A0046
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0056
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0281
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0279
Muhitimu wa shahada ya kilimo William Mbaga alibanwa kutoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali ikiwemo faida za kilimo cha 'greenhouse' pamoja na namna ambavyo maziwa ya mtindi yanapatikana. William alijieleza kwa ujasiri.
678A0157
William Mbaga akiondoka baada ya kufanya usaili.
Washiriki wenye fani na ujuzi mbalimbali walijitokeza wakiwemo madereva bodaboda, mafundi, waigizaji, waimbaji, wasusi n.k
678A0223
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0083
Waigizaji pia walikuwemo katika usaili wa #MaishaPlusMtwara
678A0167
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0113
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0308
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
678A0328
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.

678A0336
Washiriki mbalimbali waliojitokeza katika usaili wa #MaishaPlusMtwara.
Mashindano ya Maisha Plus kwa mwaka huu yanatarajia kuchukua washiriki 30 kutoka nchi za Burundi, Rwanda, Kenya, Tanzania na Uganda ambapo mshindi atajishindia ufadhili wa wazo la biashara lenye thamani ya Tzshs. Milioni 30.
"Mwaka huu washiriki wajipange sana. Maandalizi yaliyofanywa kufanikisha msimu huu hayajawahi kutokea katika historia ya Maisha Plus. Ni kama tunaanza moja" Alisema Masoud Kipanya, miongoni mwa majaji na waanzilishi wa mashindano haya.
678A0145
"Tumewekeza katika teknolojia ya kisasa ili kupata picha za matukio yenye uhalisia zaidi. Watazamaji wategemee burudani safi isiyomithirika kupitia Azam Two." Alisema David Sevuri, miongoni mwa waanzilishi wa Maisha Plus.
Taarifa mbalimbali kuhusu mashindano haya zinapatikana kupitia tovuti rasmi ya www.maishaplus.tv

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa