Home » » Kina mama changamkieni fursa Halima Dendegu

Kina mama changamkieni fursa Halima Dendegu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi Halima Dendegu amewataka kinamama mkoani Mtwara kuchangankia fursa ya kushindania shindano la Mama Shujaa wa Chakula shindano linaloendeshwa na Oxfam Tanzania.

Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo alipokuwa akishiriki katika siku ya wanawake duniani ambapo Oxfam wametumia nafasi hiyo kuzindua shindano la Mama Shujaa wa Chakula ambapo shindano hilo lilianzishwa mwaka 2011 likiwa na lengo la kumsaidia mwanamke katika kuelewa matumizi bora ya ardhi, kumiliki ardhi pamoja na kujadili masuala muhimu ya kujikomboa kwa kutumia kilimo katika jamii.

''Kinamama wa Mkoa wa Mtwara tuwe kipaumbele kwa kushiriki shindano hili muhimu katika jamii na kuhakikisha ushindi unarudi nyumbani kwetu.

Bi Dendegu pia amewapongeza Oxfam Tanzania kwa jitihada zao katika kusaidia wanawake hapa nchini kuweza kutambua umuhimu wa matumizi ya ardhi na kusaidia wengine kuweza kupata hati za ardhi hapa nchini.

Aidha Oxfam imekuwa ikifanya kazi kwa karibu na Serikali kupitia Wizara za Kilimo, Mifugo na Uvuvi, pamoja na Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi kupitia mradi wa Mama Shujaa Wa Chakula na pia kufanya kazi mbalimbali ikiwemo Ugawaji hati miliki za kimila katika vijiji vya mikoa ya Morogoro na Simiyu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa