Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Henry Mwaibambe.
Wafanyabiashara wanne, raia wa Tanzania, wameuawa
nchini Msumbiji, watatu kati yao wakipigwa risasi baada ya kuvamiwa na
watu wanaosadikiwa kuwa jambazi wenye silaha za moto na mapanga.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Mtwara, Henry Mwaibambe, alisema Watanzania hao wanaofanya biashara ya
dhahabu, walivamiwa wakiwa katika vibanda vyao vya kubadilishia fedha
usiku wa Februari 8, mwaka huu, na kushambuliwa kwa risasi na mapanga.
Alisema baadhi yao walifariki dunia papo hapo na wengine baada ya kufikishwa hospitalini.
Alisema waliouawa katika tukio hilo ni Salum Mfanga (44) mkazi wa
Temeke, Dar es Salaam, Yusuph Twalibu (34) mkazi wa Tanga, Hamisi
Mkapila (40) mkazi wa Morogoro na Mariam Ramadhan mkazi wa Tanga.
Alisema kutokana na marehemu hao kuwa sio wakazi wa Mtwara,
ilitolewa ruhusa ya kuisafirisha miili yao na baadhi ya ndugu na jamaa
ambao waliipokea miili hiyo kwa ajili ya kuisafirisha mpaka sehemu
husika kwa ajili ya shughuli nyingine za mazishi.
Doto Mfanga, ndugu wa mmoja wa marehemu hao, alisema baada ya
kutekeleza mauaji hayo, walichukua fedha ambazo thamani yake ni Sh.
milioni 20 alizokuwa nazo Salum Ramadhani pamoja na dhahabu ambazo
hazikufahamika ni za thamani gani.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment