Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais mstaafu, Benjamin Mkapa.
Mkapa alitoa onyo hilo juzi mjini hapa, wakati wa ufunguzi wa kituo
cha redio ya kijamii ya Fadhila kilichopo Wilaya ya Masasi mkoani
Mtwara.
Mkapa alisema waandishi wa habari wakiandika habari kwa usahihi,
ukweli na kwa lugha inayoeleweka kwa jamii, watasaidia kuleta maendeleo
nchini.
Alisema taaluma ya uandishi wa habari inayo fursa kubwa kuleta maendeleo ya kijamii na kisayansi.
Mkapa alisema maendeleo hayo hayawezi kuletwa kama waandishi wa
habari wataandika habari zisizo za uhakika na usahihi unaoendana na
maadili ya taaluma yao.
“Andikeni habari za ukweli zenye lugha ambayo ni sahihi maana
baadhi ya waandishi hasa katika redio za kijamii kwani bado hawatambui
namna ya matumizi ya lugha katika kuandaa habari na hata kutamka
matamshi hawatamki kwa usahihi unaotakiwa, ”alisema Mkapa.
Aliongeza kuwa baadhi ya waandishi wamekuwa wakikiuka maadili ya
uandishi kwa kuandika habari za uchochezi dhidi ya watu ili kuchafua
majina yao bila ya kufanya uchunguzi.
Kwa upande mwingine, Mkapa alikipongeza kituo hicho kwa kurusha
matangazo kwa usahihi kwa jamii iliyozungukwa na kwamba kwa sasa
kinaweza kupata habari mbalimbali za wilaya ya Masasi na maeneo mengine
ndani ya mkoa wa Mtwara na Lindi na taifa.
Naye Askofu wa Kanisa Katoliki Dayosisi ya Jimbo la Tunduru-
Masasi, Castor Msemwa, alisema waandishi wa habari wanatakiwa kuwa na
roho ya kumcha Mungu ili waweze kuandika habari katika mazingira ya
amani na utulivu.
Msemwa alisema waandishi wanapaswa kuwa huru wakati wa kutimiza
majukumu yao bila ya kuwekewa vizuizi katika kukusanya habari na pale
wanapohabarisha umma kwa masilahi ya taifa.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment