Home » » CCM MTWARA WAUNGANA KUMHAKIKISHIA USHINDI MAGUFULI

CCM MTWARA WAUNGANA KUMHAKIKISHIA USHINDI MAGUFULI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisalimia wanachama wa CCM mkoa wa Mtwara waliojitokeza kwa wingi kumsalimia kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mtwara.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akizungumza na wana CCM wa mkoa wa Mtwara nje ya ofisi za CCM mkoa.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wana CCM wa mkoa wa Mtwara nje ya Ofisi ya CCM mkoa na kuwataka wana CCM kuwa kitu kimoja na kuimarisha Chama.

 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara nje ya ofisi za CCM mkoa wa Mtwara ambapo alifika kusalimia na kusaini vitabu vya wageni.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Naibu Waziri wa Fedha Mhe.Mwigulu Nchemba.
 Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana an Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Shaibu Akwilombe.
 Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Halima Dendego akizungumza wananchi waliojitokeza kwa wingi kumsalimu Mgombea Urais wa CCM Dk.John Pombe Magufuli aliyefika ofisini hapo kutoa shukrani kwa wadhamini 231 waliomdhamini kwenye nafasi ya Urais mkoa wa Mtwara ikiwa sehemu ya kutimiza taratibu za Tume ya Taifa ya Uchaguzi.
 Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Mwigulu Nchemba akizungumza na wananchi wa Mtwara na kuwaambia Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli atashinda mapema mno.
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mtwara Ndugu Mohamed Sinani akihutubia wakazi wa Mtwara  ambapo alihakikisha kuwa Mtwara itaongoza katika kumpigia kura nyingi Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli.
Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini Husnain Murji akiwahutubia wana CCM nje ya ofisi ya CCM Mtwara na kuwaambia kuwa ushindi kwa CCM utakuwa wa kishindo .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa