Home » » MVUA KUBWA YASABABISHA MAFURIKO NA KUHARIBU MAKAZI YA WATU MKOANI MTWARA.

MVUA KUBWA YASABABISHA MAFURIKO NA KUHARIBU MAKAZI YA WATU MKOANI MTWARA.

 
Nyumba ambazo idadi yake haijaweza kufahamika mara moja zimebomoka na zingine kuingiwa na maji, miti kuanguka ovyo huku pia baadhi ya barabara katika manispaa ya Mtwara/mikindani zikijaa maji kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Mtwara.
ITV ilifika kwenye eneo la magomeni bomba la bure na kukuta baadhi ya wakazi wake wakihangaika kuyatoa maji yaliyoingia ndani ya makazi yao kutokana na mvua hiyo kunyesha siku mzima kuanzia usiku wa manane, huku maeneo mengine yakishuhudiwa wakazi wake wakihangaika kuhamisha vifaa vya ndani kuyakimbia mafuriko hayo.
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo la Magomeni Bomba la bure wamedai wamepata hasara kubwa kutokana na mafuriko hayo na kwamba yanasababishwa na barabara mpya ya chuno kuelekeza mifereji yote  ya maji kwenye makazi yao na hakuna jitihada zo zote za serikali kuwasaidia kuondokana na tatizo hilo.
  
Kwenye maeneo ya Skoya na Kyanga ITV ilishuhudia barabara zimefunikwa na mafuriko na magari yakipita kwa taabu huku wakazi wa maeneo hayo wakiiomba serikali kuwalipa fidia ya hasara na mali zao kwa kuwa mafuriko hayo yamekuwa yakijirudia rudia na serikali imeshindwa kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo.
  Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KUELEKEA UCHAGUZI 2015: JE UNAPENDA NANI AWE KIONGOZI WAKO? JAZA FOMU HII FUPI HAPA

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa