Home » » WATAKIWA KUIAMINI BIOTEKNOLOJIA

WATAKIWA KUIAMINI BIOTEKNOLOJIA

WATANZANIA wametakiwa kuiamini na kuikubali Bioteknolojia mpya ambayo itatumika katika kilimo hapa nchini na kuinua uchumi wa nchi.
Kauli hiyo imetolewa jana na Mtafiti wa Bioteknolojia nchini kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo Mikocheni Dar es Salaam, Dk. Emmarold Mneney, wakati wa mafunzo kwa wanafunzi wa chuo cha Kilimo Mati Naliendele mkoani hapa.
Dk. Mneney, alisema kuwa matumizi ya Bioteknolojia nchini bado ni mapya, ambayo ni mjumuiko wa teknolojia zinazotumia viumbe hai au sehemu ya viumbe hai kutengeneza bidhaa ama kuanzisha mchakato wa kuanzisha bidhaa.
Alisema matumizi ya Bioteknolojia yana faida kubwa katika kuongeza tija katika sekta mbalimbali za uzalishaji na za huduma za jamii kama vile, kilimo, afya, ustawi wa jamii, mazingira, maliasili na viwanda.
Katika kilimo, Bioteknolojia inaweza kusaidia kubadilisha changamoto zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi kama ukame, mafuriko, milipuko ya magonjwa na wadudu waharibifu ili kuongeza tija katika uzalishaji na ubora wa mazao.
“Matumizi ya Bioteknolojia katika sekta ya kilimo yanaweza kusaidia kukabiliana na changamoto za kilimo ili kuleta tija na kuongeza uzalishaji…Bioteknolojia hutumika katika uzalishaji wa miche bora kwa njia ya tishu, ubaini, viini vya magonjwa ya mimea, uhifadhi nasaba za mimea na uboreshaji wa mazao kwa njia ya uhandisi jeni (GMO).
 Chanzo;Tanzania daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa