Home » » WANAHABARI WAANZISHA SACCOS

WANAHABARI WAANZISHA SACCOS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
KLABU ya waandishi wa habari mkoani hapa imekamilisha hatua muhimu katika kuanzisha chama cha kuweka na kukopa kwa wanahabari na wadau wao kitakachojulikana kama Mtwara Media Saccos.
Mwenyekiti wa klabu ya waandishi wa habari mkoani Mtwara MTPC, Hassan Simba, aliwaambia waandishi wa habari ofisini kwake jana kuwa hatua iliyofikiwa sasa ni ya uandikishaji wa wanachama baada ya kukamilisha kuipitia rasmu ya katiba ya chama hicho.
Simba, alisema kuwa rasimu ya katiba hiyo iliandaliwa na kamati maalumu iliyoundwa na kupitiwa na wadau wote na sasa imekamilika na kuweza kutumika kama katiba rasmi ya chama hicho.
“Hatua ya kwanza ilikuwa kuandika katiba ambayo ilizinduliwa na mkuu wa wilaya ya Mtwara Wilman Ndile katika mkutano wa wadau uliofanyika Januari mwaka huu…baada ya hapo ilipitiwa na wanahabari na wadau wao kisha ilirejeshwa kwa kamati ambayo imeipitia na sasa ipo tayari kwa kutumika,” alisema.
Mwenyekiti huyo alisema hadi sasa wadau wamejiandikisha na kujiunga na chama hicho chenye lengo la kuwajengea uwezo kiuchumi wanahabari mkoani humo ambao wengi wao ni wale ambao hawana sifa za kupata mikopo kutoka taasisi za fedha.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa chama hicho kitakapokamilika kitakuwa mkombozi wa kiuchumi kwa wanahabari kwani kitatoa mikopo kwa masharti nafuu kwa wanachama wake.
Simba, alisema kuwa chama hicho kwa sasa kinaendeshwa chini ya uongozi wa juu wa MTPC kinatarajiwa kupata viongozi wake miezi mitatu ijayo ambapo kitafanya mkutano mkuu wa kwanza wa uchaguzi.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa