Home » » WAFANYABIASHARA WAIOMBA SERIKALI KUONGEZA KINA CHA MAJI

WAFANYABIASHARA WAIOMBA SERIKALI KUONGEZA KINA CHA MAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WAFANYABIASHARA wanaotumia kivuko cha Kilambo kilichopo wilaya ya Mtwara vijijini, mkoani Mtwara, wameiomba Serikali kuona umuhimu wa kuongeza kina cha maji katika kivuko hicho.
Wakizungumza na Tanzania Daima juzi  wafanyabiashara hao, walisema kuwa kivuko hicho kinategemea maji kutoka mto Ruvuma na Bahari ya Hindi hivyo yanapokupwa kivuko hicho kinashindwa kufanya kazi.
Alisema kivuko hicho kimekuwa kikitumiwa na wananchi wengi ambao wanafanya safari zao  kwenda Msumbiji ama Tanzania,  lakini wamekuwa wakikumbana na adha hiyo.
Mohamedi Mumbea, dereva wa gari kubwa ambaye ni Mtanzania na mfanyabiashara , alisema kuwa kutokana na kina cha maji kuwa kifupi inawalazimu kukaa kwa muda mrefu kusubiri maji.
Akizungumzia tatizo hilo, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wilman Ndile, alisema kuwa Serikali inatambua uwepo wa tatizo hilo na kuwa hivi sasa aina mpango wa kuchimba kina hicho.
Hata hivyo Ndile, alisema kuwa wawekezaji wa gesi katika mkoa huo wana mpango wa kujenga daraja katika eneo hilo ambalo linaunganisha nchi za Msumbiji na Tanzania.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa