Home » » FAWOPA YAWAWEZESHA WAZAZI, WALEZI

FAWOPA YAWAWEZESHA WAZAZI, WALEZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Faidika Wote Pamoja (Fawopa-Tanzania), la mkoani Mtwara, limeendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wazazi na walezi wa watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi ili kuwawezesha kumudu kutunza familia zao.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo siku tatu, Katibu Mtendaji wa Fawopa-Tanzania, Baltazar Komba, alisema lengo kubwa baada ya mafunzo hayo kumalizika ni kuunda vikundi vya watu kumi kumi, ambao watapewa mkopo na  Fawopa kwa ufadhili wa Serikali ya Uholanzi chini ya usimamizi wa Shirika la Maendeleo la Uholanzi la Terre Des Hommes.
“Lengo la Mafunzo haya ni kuwajengea uwezo wazazi ama walezi wa watoto waliondolewa katika ajira na wale ambao walikuwepo katika dalili za kuajiriwa… ili kuweza kuwapa mbinu za ujasiriamali jinsi ya kujitambua, kubadirisha fikra, kuthubutu, kuanzisha biashara na kuzisimamia kikamilifu bila uoga wowote ili kuweza kupata fedha za kuhudumia familia zao bila matatizo yoyote,” alisema Komba na kuongeza:
Hivi vikundi vitakavyoundwa, watakuwa wanakutana na kuchangishana mwenye uwezo wa sh 500 ama 1,000… wanachangisha na wanaweka katika sanduku fedha zao na zikifikia sh 100,000 tutawakopesha laki tano na zikifikia laki mbili tutawakopesha shilingi milioni moja na riba yake ni asilimia 3 kwa miezi sita na mkopo huo utakuwa wa miezi mitatu hadi sita.
Aidha, Komba alisema wamefanya hivyo ili kuwasaidia watoto waendelee na masomo ambayo wamewadhamini, kwa sababu mtoto akitoka chuoni ama shule, nyumbani kama hakuna mahitaji ya muhimu ya msingi atarudi mtaani tena kuendelea na biashara yake ya kuajiriwa ama kujiajiri na kujikuta anaingia katika ajira ya mapema.
“Ni lazima tuwapatie mkopo hawa wazazi, ili mwisho wa siku waweze kuwasaidia watoto wao kuwanunulia mahitaji  muhimu madogo madogo akitoka chuoni ama shule ambako Fawopa tumewapeleka kusoma, akirudi nyumbani akute mahitaji yote muhimu ya kibinadamu,” alisema.
Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, Sharifa Ismail, Mkazi wa Kata ya Reli na Salumu Ally, Mkazi wa Kata ya Vigaeni, waliishukuru Fawopa kwa kuwapa mafunzo hayo ya ujasiriamali.
“Ki ukweli tunawashukuru Fawopa kwa kutupatia haya mafunzo na wameahaidi kutupatia mikopo baada ya kumalizika kwa haya mafunzo, kinachotakiwa sasa ni sisi wenyewe wazazi ama walezi kujitahidi kwa moyo mmoja ili tuwe kitu kimoja tuweze kupata mikopo ambayo tutaweza kuwasaidia watoto wetu,” walisema na kuongeza. Hili Shirika la Fawopa ni watu wa kuigwa sana, yaani watawapeleka watoto wetu shule na chuo kuwasomesha na sisi leo tunasaidiwa mikopo lazima tuowanyeshe moyo wa dhadi kwao,” waliseama.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa