Home » » BENKI YATOA VITABU VYA MIL.1.4/-

BENKI YATOA VITABU VYA MIL.1.4/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
BENKI ya Afrika, Tawi la Mtwara imetoa msaada wa vitabu 118 vyenye thamani ya sh. milioni 1.4 kwa Shule ya Sekondari ya Bandari ya mkoani hapa.
Akizungumza mara baada ya kutoa msaada huo, Meneja wa benki hiyo, Godfrey Chilewa, alisema kuwa banki yao imekuwa ikisaidia vitabu kwa shule mbalimbali za umma zenye mahitaji ikiwa ni sehemu ya kurudisha faida walioipata kwa wananchi.
“Sisi tawi la Mtwara tuliona vema kusaidia wanafunzi wa shule yenu hasa kwa kuzingatia kuwa ni shule mpya na mna changamoto vyingi ikiwemo vitabu.
“Ndugu zangu mtakubaliana nami kwamba shule zetu nyingi hususani za umma bado zina changamoto nyingi zinazotokana na uwezo wa serikali zetu za nchi zinazoendelea kushindwa kumudu kwa asilimia 100 gharama zote za maendeleo ikiwemo elimu,” alisema.
Chilewa alisema kuwa kwa mwaka huu wamelenga kusaidia vitabu vyenye thamani ya sh.milioni 15 katika shule mbalimbali nchini na kwa miaka ijayo wataangalia miundombinu mingine lengo likiwa kusaidia shule za umma ambazo zina changamoto nyingi.
Naye Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Somoe Ismail, aliishukuru benki hiyo kwa msaada huo na kuomba watu wengine kujitokeza kuisaidia shule hiyo ambayo ni mpya ikiwa na kidato cha kwanza pekee. 
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa