Home » » MADEREVA WA BODABODA MTWARA WASITISHA MGOMO

MADEREVA WA BODABODA MTWARA WASITISHA MGOMO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MADEREVA pikipiki ‘bodaboda’ mkoani Mtwara ambao juzi waligoma kubeba abiria kupinga kitendo cha askari polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kuwakamata na kuwapiga bila sababu za msingi, jana wamerejea kutoa huduma hiyo.
Madereva hao wa bodaboda wamerejea baada ya Mkuu wa Wilata ya Mtwara, Wilman Ndile, kuwaomba waendelee kutoa huduma hiyo na yeyote aliyefanyiwa kitendo hicho aende ofisini kwake kuripoti.
Awali, akizungumza katika kituo cha redio cha Pride FM cha mjini hapa, Ndile  aliwaomba madereva hao kuendelea kutoa huduma kwa wananchi na kwamba kama kuna dereva ameshambuliwa au amepigwa na askari polisi aende katika ofisi yake au kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara kuripoti.
“Kama kweli kuna madereva wa bodaboda ambao wanalalamika  kuwa wanashambuliwa  au kupigwa na askari polisi  naomba mtu atakayefanyiwa unyama  huo afike ofisini kwangu ama kwa Kamanda wa Polisi Mkoa kuripoti.
“Baada ya kupata taarifa hiyo na kufanya uchunguzi na kujua taarifa hiyo ni ya kweli tutamchukulia hatua kali za kisheria,” alisema Ndile.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa