Home » » SHIRIKA LAIPIGA JEKI SHULE MTWARA

SHIRIKA LAIPIGA JEKI SHULE MTWARA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli la China (CPTDC) kupitia mradi wake wa ujenzi wa bomba la gesi limetoa msaada wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia pamoja na vifaa vya michezo vyenye thamani ya sh milioni tisa kwa Shule ya Msingi Msijute iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara Vijijini.
Akizungumza shuleni hapo  wakati wa hafla ya  kukabidhi msaada huo, Meneja Mradi wa kampuni hiyo, Lu Chambo,  alisema msaada huo utawasaidia wanafunzi kuinua ufaulu.
“Msaada tuliotoa utasaidia wanafunzi kuinua kiwango kikubwa cha ufaulu na mwisho wa siku tutakuja kupata wataalamu wanaoweza kufanya kazi katika sekta ya gesi na wataalamu hao watatoka hapa Mtwara,” alisema Chambo na kuwataka wanafunzi hao kusoma kwa bidii ili wawe na maisha mazuri baadaye.
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Msijute, Samli Namtanya,  aliishukuru CPTDC kwa msaada huo na kusema utaongeza ari ya ujifunzaji kwa wanafunzi na kupunguza utoro kwa wanafunzi.
  Chaanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mtwara yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa